The Uongozi Wa Kiroho Podcast-logo

The Uongozi Wa Kiroho Podcast

Religion & Spirituality Podcas

Ushauri wa kiutendaji na mafundisho ya kibiblia kusaidia kukidhi mahitaji ya Viongozi wa Kiroho

Location:

United States

Description:

Ushauri wa kiutendaji na mafundisho ya kibiblia kusaidia kukidhi mahitaji ya Viongozi wa Kiroho

Language:

Swahili


Episodes
Ask host to enable sharing for playback control

Tulee Wengine Wawe Nasi Katika Uongozi

5/18/2023
Mchungaji Cyprian Michael anatushauri juu ya uongozi wa familia na uongozi kanisani katika podcast hii. Badala ya kuongoza tukiwa peke yetu, anatuhimiza kulenga watu wenye sifa na uwezo wa kuongoza na kuwaandaa ili wawe bega kwa bega pamoja nasi katika uongozi na wawe tayari kushika uongozi wa huduma siku zijazo.

Duration:00:08:08

Ask host to enable sharing for playback control

Tufanye Uanafunzi!

3/20/2023
Mchungaji Emmanuel Mwankasole kutoka Dodoma, Tanzania anatukumbusha juu ya umuhimu wa kufanya uanafunzi. Baada ya kujibu swali la msingi "Kwa nini tufanye?" yeye anaendelea kutoa mafunzo mazuri sana kwa ajili ya viongozi, namna ya kufanya uanafunzi na faida tutakazoziona tukifanya uanafunzi kwa uaminifu. Bila shaka utabarikiwa na kujengwa na podcast hii.

Duration:00:20:37

Ask host to enable sharing for playback control

Afya Ya Kiroho

2/5/2023
Kiongozi D. Kitang'wa anatushauri kuhusu afya katika mwili wa Kristo. Ili afya ya kiroho iwe nzuri, inabidi sisi tulio viongozi wa kiroho tufundishe watu wetu vizuri. Haitoshi tu kuwafundisha kuepukana na dhambi ambazo zimekatazwa na Mungu katika Neno lake, lakini tunapaswa kuwafundisha kutii na kutenda tuliyoamriwa naye vilevile.

Duration:00:09:05

Ask host to enable sharing for playback control

Kanuni Muhimu - Seh. 1

12/3/2022
Sisi sote tuna mawazo yetu juu ya kanisa na uongozi katika kanisa, lakini mawazo yetu siyo sawa. Ni kwa sababu tumeathiriwa na mila na utamaduni pamoja na uzoefu wetu tangu utoto. Kuna aina mbalimbali za makanisa na namna tofauti tofauti za uongozi katika kanisa. Je, zote zinakubalika? Zote ni za kibiblia? Podcast hii na zingine zifuatazo zitahusu mada hii ya kanuni muhimu kutoka Neno la Mungu zinazotuongoza tuwe na kanisa la kibiblia na uongozi unaokubaliwa na Bwana.

Duration:00:16:46

Ask host to enable sharing for playback control

Kulea Viongozi Wengine

10/15/2022
Mzee Smith anazungumza na mchungaji ambaye, pamoja na kuongoza kanisa na kufanya huduma nyingine nyingi, anaweka mkazo katika kazi muhimu ya kulea viongozi wengine. Sikiliza mashauri yake namna ya kutambua viongozi wa siku zijazo na jinsi ambavyo mchungaji anaweza kuwafundisha na kuwalea katika kanisa.

Duration:00:12:49

Ask host to enable sharing for playback control

Mauti Imemezwa

8/11/2022
Tunapoomboleza kifo cha ndugu zetu, viongozi wenzetu, hebu tukumbuke mambo haya.

Duration:00:07:29

Ask host to enable sharing for playback control

Uzazi Bora

6/2/2022
Tuko na mkurugenzi wa Huruma Children’s Home katika podcast ya leo. Mzee Smith alikaa naye ili kumhoji juu ya ulezi wa watoto na vile ambavyo tunaweza kuwa wazazi bora katika ulezi wetu wa watoto. Usikose podcast hii ambayo imejaa hekima na mashauri mazuri kwa ajili yetu sisi tulio wazazi.

Duration:00:14:27

Ask host to enable sharing for playback control

Mafunzo Jangwani, Seh. ya 2

5/4/2022
Katika podcast hii tunaendelea kujifunza kutoka kwa mfano wa Musa aliyepelekwa na Bwana jangwani kwa ajili ya mafunzo. Wakati ulipowadia atoke jangwani na kuingia katika huduma alikataa, akiona hawezi. Pengine wewe unatoa udhuru kama Musa. Tuone Mungu anasemaje juu ya kiongozi aliyeweza kutumiwa naye kutenda makuu.

Duration:00:11:01

Ask host to enable sharing for playback control

Mafunzo Jangwani, Seh. ya 1

4/6/2022
Je, kiongozi mkuu ni yule ambaye ni mnenanji mzuri, ana talanta na vipaji vya pekee, na anasifiwa na watu? La, hasha. Katika mfano wa Mtumishi Musa tunaona kwamba mara nyingi ni kinyume. Kiongozi mkuu ambaye Mungu hupenda kumtumia ni yule ambaye amepita katika jangwa na kujifunza kuwa mwaminifu katika madogo, akimtegemea Bwana kwa unyenyekevu.

Duration:00:10:37

Ask host to enable sharing for playback control

Awamu Mpya

3/4/2022
Tunamkaribisha Mzee Vernon Smith ambaye anajiunga na huduma ya podcast ya Uongozi wa Kiroho na atakuwa akichangia podcast mara kwa mara.

Duration:00:11:36

Ask host to enable sharing for playback control

Agizo Kuu na Wajibu Wetu

1/28/2022
Wajibu wa kila mwamini na kila kanisa ni kutii Agizo Kuu la Yesu. Lakini kweli inawezekana katika mahali ambapo kanisa ni maskini kiuchumi na vikwazo ni vingi? Kwa njia gani mtu anayesikia wito wa kupeleka Injili kwa wasiowahi kusikia Habari Njema anaweza kujiandaa na kuenda? Maswali kama hayo ni mada ya podcast hii tunapoendelea na mahojiano na Dr. Richard Lewis.

Duration:00:16:43

Ask host to enable sharing for playback control

Agizo Kuu na Kanisa la Afrika

12/30/2021
Dr. Richard Lewis anaeleza vile ambavyo mustakabali wa huduma ya umisionari umo mikononi mwa kanisa la Marekani ya Kusini, Asia na Afrika na anatoa changamoto kwa ajili ya wasikilizaji wa podcast tuwe tayari kujibu wito wa Bwana pasipo hofu na kuongoza makanisa yetu kufundisha, kutuma na kusapoti wamisionari wanaopeleka injili kwa watu wasiowahi kusikia habari njema ya wokovu katika Yesu.

Duration:00:16:02

Ask host to enable sharing for playback control

Sifa za Kiongozi 4 - Msingi Wako

11/27/2021
Inawezekana kiongozi wa mambo ya kiroho asisome Neno la Mungu kwa uaminifu? Ndiyo. Katika podcast hii kuna mashauri na mapendekezo kwa ajili ya kiongozi wa kiroho ambaye ana moyo wa kujenga maisha na huduma yake juu ya msingi ulio bora.

Duration:00:15:22

Ask host to enable sharing for playback control

Sifa za Kiongozi 3 - Fedha ya Aibu

10/27/2021
Kila kiongozi wa kiroho anapaswa kujiuliza swali: “Kwa nini ninamtumikia Bwana?” Amini, usiamini, kuna viongozi wengi ambao wamesahau wito wao na maana yake na wameanza kufanya huduma kwa ajili ya mapato. Katika podcast hii tutaangalia Neno la Mungu kwa viongozi kupitia waraka wa Paulo kwa Timotheo. Je, unatamani fedha ya aibu?

Duration:00:15:49

Ask host to enable sharing for playback control

Sifa za Kiongozi 2 - Kauli Moja

9/2/2021
Katika podcast hii tunaendelea kukazia sifa muhimu za Kiongozi wa Kiroho. Lazima atawale ulimi wake na kutunza maneno yake na asiwe mtu wa kusengenya watu. Kiongozi awe mtu anayesema wazi, bila kuficha ficha maana yake, na asiwe mtu wa kuwasema watu wengine.

Duration:00:12:58

Ask host to enable sharing for playback control

Maisha ya Umisionari

8/2/2021
Mmisionari ambaye amekubali wito wa Bwana na kutumwa kwa watu wa lugha na utamaduni tofauti hupaswa kuzoea maisha mapya. Kuna changamoto nyingi, lakini pia kuna baraka kwa sababu ya kutii sauti ya Bwana na kumtegemea Yeye aliyemwita. Katika podcast hii tunaendelea na maongezi yetu na Mmisionari Daudi Likama na kusikia ushuhuda wake juu ya maisha na huduma yake Msumbiji. Bwana atumie ushuhuda wake ili kutuhimiza sisi sote na kufanya masikio yetu tayari kusikia wito wa Bwana kwa ajili yetu.

Duration:00:18:27

Ask host to enable sharing for playback control

Kuitikia Wito wa Umisionari

7/2/2021
Wengi walisema “haiwezekani!” Walidai kwamba Tanzania ni nchi maskini na kuna haja ya wamisionari kuja Tanzania na kuleta Injili. Lakini Mmisionari Mtanzania kutumwa na kanisa la Tanzania na kupeleka Injili nje si rahisi. Lakini Bwana aliita na Ndugu Likama aliitika. Jiunga nasi katika podcast hii na ijayo ili kusikia ushuhuda wa Ndugu Daudi Likama aliyetumwa na kanisa lake kupeleka habari njema ya wokovu Msumbiji.

Duration:00:18:15

Ask host to enable sharing for playback control

Sifa za Kiongozi 1- Msimamo

2/15/2021
Walio viongozi kweli kweli si viongozi wa jina tu, bali ni viongozi waliostahili kuongoza kutokana na msimamo wao na uaminifu wao mbele za Mungu na mbele ya watu. Katika podcast hii ya na podcast zifuatazo tutaangalia sifa za muhimu ambazo humfanya mtu awe kiongozi mwaminifu aliyetumiwa na Bwana kuongoza wengine vema.

Duration:00:17:21

Ask host to enable sharing for playback control

Hekima Kutoka Kwa Kiongozi Mwanamke

1/30/2021
Sikiliza mashauri na hekima ya mwanamke mwaminifu ambaye amekuwa kiongozi wa kiroho siku nyingi. Katika podcast hii tunamwuliza juu ya familia yake, huduma yake, baraka na changamoto anazoziona katika uongozi wake n.k. Podcast hii si tu kwa ajili ya akina dada. Kiongozi mwanamume, sisi pia tunahitaji hekima hii kutoka kwa Mama Moses. Karibu tusikilize!

Duration:00:13:06

Ask host to enable sharing for playback control

Ubora wa Viongozi Wanawake

1/15/2021
Je, ni lazima mwanamke awe nyuma ya mwanamume katika ulimwengu wa uongozi? Wanawake wanafaa tu kusaidia waume zao na wanaume wengine, au wanawake wanafaa kuongoza wenyewe katika mambo ya kiroho? Katika podcast hii tunaongea na wanawake waaminifu walio viongozi wenyewe. Ni wake wa wachungaji na wasaidizi wa waume zao katika huduma. Lakini hawa wanawake ni zaidi ya wasaidizi. Wenyewe wanaongoza katika huduma na wao wenyewe ni viongozi katika mambo ya kiroho.

Duration:00:22:51