Roho Mtakatifu akaaye ndani yangu - Njia ya tahadhari kwako katika kumpokea Roho Mtakatifu-logo

Roho Mtakatifu akaaye ndani yangu - Njia ya tahadhari kwako katika kumpokea Roho Mtakatifu

Religion & Spirituality Podcasts

Katika Ukristo nyakati hizi, mojawapo ya mambo yanayozungumziwa mara nyingi ni kuhusiana na habari za "wokovu toka dhambini" na "kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu". Hata hivyo ni watu wachache walio na ufahamu ulio sahihi wa mambo haya mawili, ingawa ukweli ni kwamba haya ni mabo mawili muhimu kuhusiana na maswala ya Ukristo. Mbaya ni nini, bado hatujaweza kupata maandiko yanayo tufunza kwa uwazi juu ya mambo haya yaliyo tajwa hapo juu. Wapo watunzi wa vitabu wa Kikristo walio wengi wakitukuza karama za Roho Mtakatifu au kuelezea maisha ya kujazwa na Roho. Lakini hakuna hata mmoja kati yao anaye thubutu kushughulika na swali la msingi,nalo ni "Kwa namna gani anaye amini ataweza kumpokea Roho Mtakatifu kwa uhakika?" Kwanini? Ukweli wa kushangaza ni kwamba hawajaweza kuandika kwa viwango vilivyo kamili kwa sababu hawakuweza kuwa na ufahamu ulio kamili juu ya hili. Kama vili Nabii Hosea alipo paza sauti na kusema "Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa", kwa nyakati hizi si wakristo wachache wanao vutwa katika ushabiki wa kidini, wakitegemea kumpokea Roho Mtakatifu. Huamini kwamba wataweza kumpokea Kumpokea Roho Mtakatifu baada ya kufikia kiwango cha hisia kali na mashamusham. Lakini si swala la kutia chumnvi tukisema kwamba kinacho itwa imani na watu hawa ndicho kinacho fanya Ukristo udharaulike na hata kuonekana kama mojawapo tu ya dini mfano Shama (Shamanism), na ukereketwa wa aina hii unatoka na Shetani Mtunzi, Mchungaji Paul C. Jong huthubutu siku zote kutangaza ukweli. Hujihusisha na maswala yaliyo muhimu kwa kiwango cha kutosha, ambacho wengi wa watunzi wa vitabu vya kiroho wamekwepa kwa muda mrefu. Kwanza amefafanua maana ya "kuzaliwa upya mara ya pili" na "kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu" na kuelezea uhusiano usio kwepeka kati ya mambo yaha mawili ya ngozo za msingi. Na ndipo basi akachukua maelezo ya kina kwa pamoja kuhusiana na Roho Mtakatifu, kuanzia "namna ya utambuzi war oho" kuelekea "namna ya kuishi maisha ya ujazo wa Roho". Kwa habari zaidi mwandishi anakushauri uchunguze yaliyomo katika kitabu hiki ambayo yamewekwa katika kurasa za tovuti hii. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Location:

United States

Description:

Katika Ukristo nyakati hizi, mojawapo ya mambo yanayozungumziwa mara nyingi ni kuhusiana na habari za "wokovu toka dhambini" na "kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu". Hata hivyo ni watu wachache walio na ufahamu ulio sahihi wa mambo haya mawili, ingawa ukweli ni kwamba haya ni mabo mawili muhimu kuhusiana na maswala ya Ukristo. Mbaya ni nini, bado hatujaweza kupata maandiko yanayo tufunza kwa uwazi juu ya mambo haya yaliyo tajwa hapo juu. Wapo watunzi wa vitabu wa Kikristo walio wengi wakitukuza karama za Roho Mtakatifu au kuelezea maisha ya kujazwa na Roho. Lakini hakuna hata mmoja kati yao anaye thubutu kushughulika na swali la msingi,nalo ni "Kwa namna gani anaye amini ataweza kumpokea Roho Mtakatifu kwa uhakika?" Kwanini? Ukweli wa kushangaza ni kwamba hawajaweza kuandika kwa viwango vilivyo kamili kwa sababu hawakuweza kuwa na ufahamu ulio kamili juu ya hili. Kama vili Nabii Hosea alipo paza sauti na kusema "Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa", kwa nyakati hizi si wakristo wachache wanao vutwa katika ushabiki wa kidini, wakitegemea kumpokea Roho Mtakatifu. Huamini kwamba wataweza kumpokea Kumpokea Roho Mtakatifu baada ya kufikia kiwango cha hisia kali na mashamusham. Lakini si swala la kutia chumnvi tukisema kwamba kinacho itwa imani na watu hawa ndicho kinacho fanya Ukristo udharaulike na hata kuonekana kama mojawapo tu ya dini mfano Shama (Shamanism), na ukereketwa wa aina hii unatoka na Shetani Mtunzi, Mchungaji Paul C. Jong huthubutu siku zote kutangaza ukweli. Hujihusisha na maswala yaliyo muhimu kwa kiwango cha kutosha, ambacho wengi wa watunzi wa vitabu vya kiroho wamekwepa kwa muda mrefu. Kwanza amefafanua maana ya "kuzaliwa upya mara ya pili" na "kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu" na kuelezea uhusiano usio kwepeka kati ya mambo yaha mawili ya ngozo za msingi. Na ndipo basi akachukua maelezo ya kina kwa pamoja kuhusiana na Roho Mtakatifu, kuanzia "namna ya utambuzi war oho" kuelekea "namna ya kuishi maisha ya ujazo wa Roho". Kwa habari zaidi mwandishi anakushauri uchunguze yaliyomo katika kitabu hiki ambayo yamewekwa katika kurasa za tovuti hii. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Language:

Swahili


Episodes
Ask host to enable sharing for playback control

1. Roho Mtakatifu Hufanya kazi kupitia ahadi ya Neno la Mungu (Matendo 1:4-8)

1/13/2023
Hapo mwanzo nilipatwa na tukio la kujiwa na miale ifananayo kama Roho Mtakatifu wakati wa maombi. Lakini miale hii haikudumu kwa muda, hivyo punde ilitoweka mbele ya kitita cha dhambi. Ingawa leo napenda kukuonyesha ukweli kuhusu Roho Mtakatifu ambaye atakaye kaa ndani yetu hata milele, si kwakupitia roho zidanganyazo ambazo hutambulika kwa dhambi, bali kupitia injili ya kweli. Roho Mtakatifu nitakaye mtambulisha kwako kwa kupitia ujumbe huu si kitu fulani unacho weza kupokea kwa maombi bali kupitia imani katika injili ya majina Roho tu. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:16:22

Ask host to enable sharing for playback control

2. Je, inawezekana mtu kumnunua Roho Mtakatifu kwa uwezo wake? (Matendo 8:14-24)

1/13/2023
Husika na somo kuu katika kifungu hiki, napenda kuleta ujumbe huu iwapo “mtu anaweza kumpokea Roho Mtakatifu ndani yake kwa kupitia juhudi binafsi”. Mitume katika nyakati hizo za Kanisa la kwanza waliweza kupokea nguvu toka kwa Mungu na kutumwa sehemu kadhaa naye. Yapo matendo ya miujiza kadhaa katika Kitabu cha Matendo, mojawapo likiwa kushuka kwa Roho Mtakatifu juu ya waumini pale Mitume walipowawekea mikono. Biblia inasema “Mitume walipowawekea mikono wale ambao hawakuwa wamempokea Roho Mtakatifu ingawa walikwisha mwamini Yesu, walipokea Roho Mtakatifu.” https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:57:06

Ask host to enable sharing for playback control

3. Mlimpokea Roho Mtakatifu mlipoamini? (Matendo 19:1-3)

1/13/2023
Aina gani ya Injili Paulo alihubiri? Alihubiri Injili ya ubatizo wa Yesu na damu yake. Matendo 19:1-2 inasema “Ikiwa, Apolo alipokuwa Korintho, Paulo akiisha kupita kati ya nchi za juu akafika Efeso, akakutana na Wanafunzi kadhaa wa kadha huko akawauliza, Je, mlimpokea Roho Mtakatifu mlipoamini?” Hata hivyo watu hawa walikuwa wamekwisha mwamini Yesu huku wakiwa wameweka kando maana ya ubatizo wa Yesu. Hawakujua juu ya Injili njema ambayo hupelekea kumpokea Roho Mtakatifu ndani. Na hii kupelekea Paulo kuuliza “Je, mlimpokea Roho Mtakatifu mlipoamini?” lilikuwa swali geni kwa baadhi ya wafuasi. Watu wengine wangeliweza kuuliza “Je, una mwamini Yesu?” Lakini Paulo aliuliza swali katika njia isiyokuwa ya kawaida ili kwamba waweze kumpokea Roho Mtakatifu, ndani yao kwa kufanya upya imani zao katika Injili njema. Huduma ya Paulo ilikuwa ni kuhubiri Injili njema ya ubatizo wa Yesu kwa Yohana Mbatizaji. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:19:03

Ask host to enable sharing for playback control

4. Wale walio na imani sawa na Mitume (Matendo 3:19)

1/13/2023
Kwa kuangalia wafuasi wa Yesu Kristo kiwango cha imani zao walipokuwa na Roho Mtakatifu ndani yao ni tofauti kabisa na imani zao walipokuwa hawajawa na Roho huyo. Miili yao haikuonekana kuwa tofauti lakini baada ya kumpoke Roho Mtakatifu maisha yao yalibadilika kabisa kwa nuru ya Yesu Kristo. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:25:37

Ask host to enable sharing for playback control

5. Je, unataka kuwa na Ushirika na Roho Mtakatifu? (1 Yohana 1:1-10)

1/13/2023
Ikiwa unahitaji kuwa na usharika na Roho Mtakatifu kwanza kabisa lazima uelewe kwamba dhambi iliyo ndogo kabisa mbele ya Mungu inatosha kutokufanya usharika na Mungu. Unaweza kudhani “Sasa itawezekanaje mtu asiwe na dhambi hata kidogo mbele ya Mungu?” Lakini ikiwa kweli unatamani usharika na Bwana basi lazima pasiwepo na kiza moyoni mwako. Hivyo ili uwe na usharika na Bwana, unahitajika kujua kwamba lazima uamini Injili ya ukombozi na kujitakasa dhambi zako zote. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:40:50

Ask host to enable sharing for playback control

6. Amini ili Roho Mtakatifu akae ndani yako (Mathayo 25:1-12)

1/13/2023
Katika kifungu kilichopita hapo juu tumeona wanawali watano wenye busara na wapumbavu, wanawali wapumbavu waliwaomba wale wenyebusara kuwagawia kiasi cha mafuta ya taa lakini wenye busara wakawajibu wale wapumbavu “hayatatutosha sisi na ninyi shikeni njia muende kwa wauzao mkajinunulie”. Hivyo wakati wale walio wapumbavu wakienda nje kununua mafuta hayo, wale wenye busara walikuwa nayo katika taa zao na kuingia katika sherehe za harusi. Sasa basi ni kwa namna gani tunaweza kuyatayarisha mafuta kwa ajili ya Bwana? Kitu pekee tunachoweza kufanya ni kuusubiri msamaha wake wa dhambi katika mioyo yetu. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:29:24

Ask host to enable sharing for playback control

7. Injili iliyo njema inayowezesha Roho Mtakatifu kukaa ndani ya wanao amini (Isaya 9:6-7)

1/13/2023
Ili kumpokea Roho Mtakatifu tunahitajika kuwa na imani katika injili ya maji na Roho. Bwana wetu ameitwa wa Ajabu, Mshauri na Mungu mwenye Enzi. Bwana wetu amejitambulisha ndiye njia ya kwenda Mbinguni. Yesu Kristo amempatia kila mmoja zawadi ya Inijili njema. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:56:58

Ask host to enable sharing for playback control

8. Kupitia nani maji ya uzima ya Roho Mtakatifu hutiririka? (Yohana 7:37-38)

1/13/2023
Maji ya uzima ya Roho Mtakatifu hutiririka toka mioyo ya wale wote wanao amini injili njema. Yohana 7:38 inasema “Aniaminiye mimi kama vile maandiko yalivyonena mito ya maji yaliyo hai itatiririka ndani yake.” Maana yake ni kwamba upo wokovu wa kweli na ondoleo la dhambi kwa wale wote wenye kuamini injili njema ambayo Mungu ametupatia. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:46:41

Ask host to enable sharing for playback control

9. Injili ya ubatizo wake iliyo tutakasa (Waefeso 2:14-22)

1/13/2023
Kwanini tunatengwa na Mungu, na ni kwasababu gani hatuwezi kumjongelea kwa karibu? Yule mwanake aliye rithiwa alikuja kugundua yakwamba mama yake mzazi alimtelekeza hata kufikia kurithiwa ili aweze kumkomboa tokana na ufukara. Nini kingeliweza kututenganisha na Mungu? Jibu ni kwamba, shetani alipo mjaribu mwanadamu kutenda dhambi ndipo hapo dhambi hiyo ilipotutenga na Mungu. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:25:17

Ask host to enable sharing for playback control

10. Tembea katika Roho! (Wagalatia 5:16-26, 6:6-18)

1/13/2023
Mtume Paulo aliandika juu ya Roho Mtakatifu katika Waraka kwa Wagalatia. Katika Wagalatia 5:13-14 alisema “Maana ninyi, ndugu mliitwa mpate uhuru lakini uhuru wenu usiwe sababu ya kuufuata mwili bali tumikianeni kwa upendo. Maana torati yote imetimilika katika neno moja nalo ni hili, Umpende jirani yako kama nafsi yako”. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:40:30

Ask host to enable sharing for playback control

11. Kutunza maisha yaliyo na ujazo wa Roho Mtakatifu ndani yako (Waefeso 5:6-18)

1/13/2023
Ili “kuyatunza maisha yaliyo na ujazo wa Roho Mtakatifu” ni lazima tujitolee katika kuihubiri injili. Ili kuishi maisha yaliyo na ujazo wa Roho Mtakatifu yatupasa kwanza kupokea baraka ambayo ndiyo huleta uwepo wa Roho Mtakatifu ndani ya mioyo yetu. Ili kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu ni lazima tuwe na imani ambapo ni kuamini injili ya maji na Roho Mungu aliyotupatia na kwa kuwa na imani hii tutapokea baraka ambayo humfanya Roho Mtakatifu kuweka makazi ndani yetu. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:36:05

Ask host to enable sharing for playback control

12. Kuishi Maisha ya Ujazo wa Roho Mtakatifu (Tito 3:1-8)

1/13/2023
Wale wote wenye kumwamini Yesu na kuwa na uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yao lazima waishi maisha ya ujazo wa Roho Mtakatifu. Kwa Wakristo maisha ya ujazo wa Roho Mtakatifu ndiyo mahitaji ya Mungu. Inatulazimu kufuata mpangilio wake. Hivyo basi, kwa vipi tutaweza kuishi maisha ya ujazo wa Roho Mtakatifu? Nilazima tuwe makini kwa lile Mtume Paulo aliloelezea. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:41:11

Ask host to enable sharing for playback control

13. Kazi na vipawa vya Roho Mtakatifu (Yohana 16:5-11)

1/13/2023
Katika Mwanzo 1:2 imeandikwa, “Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu na giza lilikuwa juu ya uso wa maji”. Tunaweza kuona toka katika kifungu hiki kwamba Roho Mtakatifu hakai ndani ya mioyo iliyo jawa na vurugu na dhambi bali hukaa katika mioyo ya wale wenye kuiamini injili njema tu. Hata hivyo watu wengi kwa vurugu zao na utupu wa mioyo chini ya imani za matendo ya kimashamshamu, husema kwamba wanataka kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu huku wakiwa na dhambi mioyoni mwao. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:27:06

Ask host to enable sharing for playback control

14. Ipi toba ya kweli katika kumpokea Roho Mtakatifu? (Matendo 2:38)

1/13/2023
Biblia inasema katika (Matendo 2) kwamba mahubiri ya Petro yaliwagusa kwa undani watu na hata kuwasababisha watubu dhambi zao. Walichomwa mioyo yao na kumwambia Petro na mitume wengine, “Tutendeje ndugu zetu? Petro akawaambia tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kisto mpate ondoleo la dhambi zenu nayinyi mtapokea kipawa cha Roho Mtaakatifu” (Matendo 2:38). https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:14:49

Ask host to enable sharing for playback control

15. Utaweza kupokea ujazo wa Roho Mtakatifu pale utakapo elewa kweli tu (Yohana 8:31-36)

1/13/2023
Je unaelewa ukweli ulivyo? Yesu alisema “mimi ndimi njia” (Yohana 14:6), hivyo kumjua Yesu ndiko kuijua kweli. Je, Roho Mtakatifu huweka makazi ndani yako kwa kuishukuru imani ya injili njema? Imekupasa ugundue kwamba ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani ni taswira ya injili njema. Hivyo imekupasa kuiamini hivyo. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:06:50

Ask host to enable sharing for playback control

16. Mikakati ya wanao mpokea Roho Mtakatifu (Isaya 61:1-11)

1/13/2023
Mtu aliye kwisha mpokea Roho Mtakatifu yampasa kufanya nini? Imempasa kuihubiri injili ya maji na Roho kwa watu wote. Mungu ameweka dhamana ya injili njema yakuzaliwa upya mara ya pili kwa maji na kwa Roho mikononi mwa wale wote walio kwisha kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu.Wale wote walio kwisha pokea msamaha wa dhambi zao mbele ya Mungu hupokea Roho Mtakatifu. Sasa basi kwanini unadhani Mungu ametunuku karama ya Roho Mtakatifu kwao? https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:19:19

Ask host to enable sharing for playback control

17. Yatupasa tuwe na imani na tumaini katika Roho Mtakatifu (Warumi 8:16-25)

1/13/2023
Je, lipo tumaini la ulimwengu wa leo? Hapana Hakuna. Lipo kwa Yesu tu. Sasa ni wakati usio tabirika na kukosa matumaini. Kila kitu kinabadilika kila siku na kwa kasi watu wanajaribu kwa bidii kwenda sambamba na badiliko yaendayo kasi. Hawatafuti ukweli wa kiroho au hata kuhusika na faraja ya kiroho. Badala yake wanahangaikia kuzuia kushindwa na kuishia kuwa watumwa wa ulimwengu. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:17:13

Ask host to enable sharing for playback control

18. Ukweli uongozao wanao amini kujazwa Roho Mtakatifu (Yoshua 4:23)

1/13/2023
Ningependa sasa nizungumzie injili njema ya kweli inayotuwezesha kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu. Baada ya kifo cha Musa, Mungu katuletea Yoshua kuiongoza Israeli. Musa alikuwa ni mwakilishi wa sheria katika Agano la Kale. Ikiwa Musa angelivuka mto wa Yordani akiwa na wana wa Israel na kuingia Kanani pasingelikuwepo na umuhimu wa Yoshua kuwa kiongozi wa watu. Hata hivyo Mungu alimwezesha Musa kufika eneo lile karibu na ardhi ya Kanani na kumzuia asiingie. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:23:43

Ask host to enable sharing for playback control

19. Injili njema Iliyo pasua pazia la Hekalu (Mathayo 27:45-54)

1/12/2023
Ili kuelewa ukweli wa injili hii njema, imempasa mtu kwanza kujua na kuelewa juu ya mpangilio wa utoaji dhabihu ulivyokuwa ukifanywa katika kusamehe watu dhambi zao mbele ya Mungu nyakati zile za Agano la Kale. Yatupasa kujua na kuamini ukweli ufuatao. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:23:31

Ask host to enable sharing for playback control

20. Mtu aliye na uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yake ndiye aongozaye wengine katika kumpokea Roho Mtakatifu (Yohana 20:21-23)

1/12/2023
Yohana sura 20 inahabari ya ufufuko wa Yesu. Bwana wetu alifufuka tena toka kifoni na kuwaeleza wafuasi wake “Pokeeni Roho Mtakatifu”. Wafuasi wa Yesu walipokea uwepo wa Roho Mtakatifu kama zawadi toka kwake. Yesu alitoa uwepo wa Roho Mtakatifu na uzima wa milele kwa wale wote wanaoamini ubatizo wake na damu yake iliyo safisha dhambi zao zote. Biblia inasema kwamba ubatizo wa Yesu ni mfano wa wokovu ambapo ubatizo huo uliokoa wanadamu wote kwa dhambi zao (1 Petro 3:21). https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

Duration:00:34:09